MWILI wa Mwenyekiti wa Chama cha Tanzania Labour Party (TLP) Agustino Lyatonga Mrema unatarajiwa kuzikwa Alhamisi tarehe 25 Agosti, 2022 nyumbani kwake Kiraracha- Marangu mkoani Kilimanjaro. Anaripoti Juliana Assenga, TUDARCo … (endelea).
Msemaji wa familia ya Mzee Mrema, Profesa Alex Mrema amewaeleza waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam kuwa mwili wa mwasiasa huyo mkongwe aliyewahi kuwa waziri wa mambo ya ndani ya nchi, utaagwa katika Kanisa Katoliki Mbezi Salasala jijini Dar es Salaam kisha kusafirishwa kuelekea Marangu mkoani Kilimanjaro kwa ajili ya maziko.
Amesema chanzo cha kifo chake mwanasiasa huyo ni tatizo la mapafu.
Mrema alifariki jana asubuhi tarehe 21 Agosti, 2022 katika Hospitali ya Taifa Muhimbili alikokuwa amelazwa tangu tarehe 16 Agosti, 2022.
Leave a comment