MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Barcelona raia wa Poland, Robert Lewandowsik amefungua rasmi akaunti ya mabao katika klabu yake mpya baada ya jana tarehe 21 Agosti, 2022 kufunga mabao mawili katika ushindi wa mabao manne kwa moja dhidi ya Real Sociedad. Anaripoti Damas Ndelema, TUDARCo … (endelea).
Mchezaji huyo aliyejiunga na miamba hiyo ya Hispania akitokea Ligi kuu ya Ujerumani katika klabu ya Bayern Munich, mechi hiyo inakuwa ni ya pili kuitumikia miamba hiyo baada ya mechi ya kwanza kuisha kwa suluhu ya bila kufungana na Rayo Vallecano hivyo jana amefungua rasmi akaunti yake ya mabao.
Barcelona mpaka sasa wamecheza michezo miwili na kujikusanyia alama nne huku mashabiki wengi wa timu wakitarajia kupata matokeao mazuri kulingana na usajili wao walioufanya baada ya msimu uliopita kuisha bila kutwaa kikombe.
Mahasimu wao Real Madrid walitawala msimu huo kwa kubeba kombe la ligi kuu pamoja na Ligi ya mabigwa barani Ulaya
Aidha, mpaka sasa vita ya kuwania tuzo ya mfungaji bora inatazamiwa kuwa kali tangu mchezaji huyo ajiunge na Barcelona.
Lewandowsik anatarajia kukutana na upinzani mkubwa kutoka kwa mtaalamu wa kupachika mabao na mfungaji bora wa msimu uliopita Karim Benzema anaeitumikia klabu ya Real Madrid
Leave a comment