Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Methanol yabainika chanzo vifo vijana 21
Kimataifa

Methanol yabainika chanzo vifo vijana 21

Spread the love

 

CHANZO cha vijana 21 waliopoteza maisha mwezi Juni huko nchini Afrika Kusini katika klabu moja ya usiku, imebainika kuwa ni sumu aina ya Methanol. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea). 

Kwa mujibu wa Naibu mratibu wa huduma za afya kwenye jimbo la Eastern Cape nchini humo, Daktari Litha Matinawe amesema kemikali hatari aina ya methanol huenda ilisababisha vifo vya vijana 21 waliokuwa wakisherehekea kumaliza mitihani yao ya elimu ya juu.

Kwa mujibu wa shirika la habari la AP, kemikali hiyo ilipatikana kwenye kila mwili wa waathirika hao baada ya kufanyiwa uchunguzi, wakati wataalam wakiendelea kubaini iwapo viwango vilivyopatikana vilitosha kusababisha vifo hivyo.

Vijana hao ambao wengi walikuwa wanafunzi walifariki wakati wakiwa ndani ya klabu kimoja cha usiku mjini humo.

Methanol ni kemikali yenye uwezo wa kulevya na ambayo hutumika kwenye viwanda au kutengeneza dawa za wadudu na wala sio pombe ya kutumiwa na wanadamu.

Vijana hao waliokuwa na umri kati ya miaka 13 na 17 walipatikana wakiwa wamekufa kwenye klabu hiyo, miili yao ikiwa imetapakaa kila mahali.

Polisi wa Afrika kusini wanasubiri matokeo kamili ya uchunguzi, ili kubaini ni nani atakaye funguliwa mashitaka kutokana na mkasa huo wenye kusikitisha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!