Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Samia aunda Kamati kufumua vyombo vya haki jinai
Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia aunda Kamati kufumua vyombo vya haki jinai

Rais Samia Suluhu Hassan
Spread the love

 

RAIS Samia Suluhu Hassan ameunda Kamati ya watu 12 na sekretarieti ya watu watano kwaajili ya kuchunguza na kumshauri muundo mzuri wa vyombo vya haki jinai. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Rais Samia amebainisha hay oleo Jumatano tarehe 20 Julai, 2022, mara baada ya kuwaapisha viongozi mbalimbali akiwemo Inspekta Jenerali wa Jeshi la Polisi, Camilius Wambura.

Mkuu huyo wa nchi amesema Kamati hiyo itaongozwa na Jaji Mkuu Mstaafu, Othman Chande akisaidiwa na Makamu Mwenyekiti Ombeni Sefue na kwamba wajumbe wengine watafahamika baadae.

“Nimeunda kamati kunishauri namna ya kuleta mabadiliko ya utendaji kazi wenye matokeo bora kwenye vyombo vyetu vya haki jinai, kwahiyo tutaanza na polisi tukimaliza wataleta mapendekezo, tunakwenda majeshi mengine yote,” amesema Rais Samia.

“Serikali sasa tunakuja na jicho jingine ndani ya vyombo vya ulinzi na usalama Tanzania, tunakwenda kusimamia haki, hii kamati yangu itaniletea mrejesho kila jeshi linapomaliza kuchunguzwa na kufanyiwa maboresho, tutakuja na miundo inayofaa sasa hivi ili kujenga majeshi imara na bora kutumikia watanzania,” amesisitiza.

Rais Samia amempongeza IGP Wambura kwa kazi ambazo amefanya ndani ya polisi muda wote na kwa kuteuliwa katika nafasi hiyo, “nachotegemea ni kuona mabadiliko, ufanisi, usalama wa raia na mali zao unaimarika ndani ya Jeshi la Polisi.”

Samia amesema katika “dhana” ya utawala bora suala la haki kwa wananchi “linapaswa kupewa kipaumbele kikubwa kwa maana hiyo nimeamua kufanya mabadiliko ya mfumo kwenye taasisi zetu za haki jamii.”

Amezitaja taasisi hizo kuwa ni Jeshi la Polisi, Ofisi ya Mashitaka, TAKUKURU, Jeshi la Magereza na Mamlaka ya kupambana na dawa za kulevya, “zote lazima tufanyie marekebisho kwa kuangalia miundo ikoje, je inasaidia leo inaleta ufanisi leo, inakwenda na yaliyopo duniani?”

Samia amesema katika mabadiliko hayo wataangalia mifumo ya ajira, mafunzo, maadili na nidhamu sambamba na kuangalia mifumo ya utendaji kazi.

“Lazima tuangalie tunakwendaje, tunakwenda kama kanuni zinavyotutaka, kama sheria zinavyosema, au tumezoeana mno kiasi ambacho tunafanya tu na hatuwezi kuchukuliana hatua yeyote,” amesema.

Ameongeza kuwa licha ya kuwa kuna taasisi zinazojitahidi kuchukua hatua lakini amekuwa akipokea lawama kutoka kwa wanaochukuliwa hatua.

“Ukiuliza kafanya nini kafukuzwa, unaletewa mambo unasema tena ulichelewa kumfukuza.”
Mbali na hayo amesema wanakwenda kuangalia mifumo ya upandishaji vyeo na kuhakikisha wanaopandishwa wanakuwa na sifa.

Pia amesema upatikanaji wa watendaji kazi utaangaliwa kwa kuhakikisha wanaochaguliwa kujiunga na vyombo hivyo wanakuwa na sifa pamoja na kufaulu mafunzo ipasavyo.

1 Comment

  • Rais Samia. Hongera! Mara 99%.Mungu akuruzuku nyingi elimu yakuona (yenye manufaa kwa umma) sambamba na busara tele.kwa kuwajali wanyonge. KAMATI KUFUMUA VYOMBO VYA HAKI JINAI.itakapo kamilika sambamba na mapendekezo. Iwe dira kwa wakuu Wa wa mikoa na wilaya kufanya Nazi ya kuondoa dhulma na ubadhilifu wa Mali ya watanzania. Takriban zaidi ya miaka 3 iliyopita Mh.waziri mkuu K.Majaliwa.aliunda kamati kushughulikia kero ya nyumba viwanja na mashamba sambamba na kutoa mapendekezo.cha kuhuzunisha. jeshi la polisi ofisi ya mashitaka na Takukuru baadhi ya watuhumiwa hawajapelekwa mahakamani kwa kesi ya kugushi hati-miliki ya kiwanja

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!