Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Meli ya mizigo yazama pwani ya Ukreini baada ya mlipuko
Kimataifa

Meli ya mizigo yazama pwani ya Ukreini baada ya mlipuko

Spread the love

 

WAMILIKI wa meli kutoka Estonia wamesema meli yao imezama katika pwani ya Ukreini baada ya kutokea mlipuko. Inaripoti BBC … (endelea).

Wamiliki hao wamesema watumishi wawili wa meli hiyo waliokolewa na wengine wanne walipotea kwa muda na baadaye wote kuokolewa na timu ya uokozi ya Ukreini.

Meli hiyo inayopeperusha bendera ya Panama inamilikiwa na kampuni ya Vista yenye makao yake Estonia ambayo ni mwanachama wa Umoja wa Kujihami NATO na inapakana na Urusi.

Meli hiyo iliingia Pwani ya Ukreini baada ya siku chache zilizopita kuondoka katika bandari ya Chornomorsk karibu na Odesa. Hata hivyo bado haijajulikana sababu ya mlipuko huo.

Jeshi la Ukreini limesema Urusi imekuwa ikituma manuari kwa lengo la kuiteka Odesa, jiji la watu zaidi ya milioni moja na lenye bandari muhimu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!