Saturday , 11 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbunge Kubenea kuhojiwa Polisi Dar 
Habari za Siasa

Mbunge Kubenea kuhojiwa Polisi Dar 

Saed Kubenea, Mbunge wa Ubungo
Spread the love

MBUNGE wa Jimbo la Ubungo (Chadema), Saed Kubenea  amemtaka mwenyekiti wa Chama cha Wananchi (CUF), anayetambulika na Msajili wa Vyama Vya Siasa Nchini Profesa Ibrahim Lipumba kuacha kulipotezea muda Jeshi la Polisi na kwamba aliache lifanye kazi yake , anaandika, Irene David.

Kauli hiyo ya Kubenea ikiwa ni siku moja baada ya Profea Lipumba kukimbilia Polisi Kanda maalum ya  Dar es salaam, akilalamika kwamba anatishiwa na mwanasiasa kutolewa katika ofisi yake iliyopo Buguruni jijini Dar es Salaam.

Wasiwasi huo umeibuka mara baada ya Uongozi wa Kanda ya Pwani na Dar es salaam (Chadema)  na viongozi wa CUF wanaomuuunga mkono Maalim Seif  wakiongozwa na Kubenea, wiki iliyopita kuanzisha operesheni ya Ondoa Msaliti Buguruni(OMB), kwa lengo la kumng’oa Profesa Lipumba ambaye ni msaliti.

Akizungumza na MwanaHALISI Online, Kubenea amesema amepokea wito wa polisi kwa njia ya simu na kwamba kesho mchana ataripoti polisi, lakini pia ameongeza kuwa kwa namna yoyote  ile hatayumbishwa mpaka ahakikishe wanamng’oa ofisini msaliti huyo.

“Bado adhima ya kumwondoa msaliti Buguruni ipo palepale na haiwezi kurejeshwa nyuma kwa maneno rejareja na ahadi za uongo ama vitisho vya aina yoyote,”

“Lipumba ni msaliti ni lazima aondoke na katika hili ntauza hata kiatu changu lakini ataondoka.” amesema Kubenea.

Pomoja na hayo kubenea amesema, tayari matawi ya Chechinia, Hosigofina, Palestine, Kosovo, Saratoga, Arafati yote yameonyesha nia ya kumuunga mkono

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Vijana UVCCM Kagera wataka mwenyekiti wao ajiuzulu

Spread the loveVIJANA wa Chama cha Mapinduzi Mkoa wa Kagera wamemtaka Mwenyekiti...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina awavaa mawaziri wanaompelekea majungu Rais Samia

Spread the loveMBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina (CCM) amewataka baadhi ya mawaziri...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

THRDC, Wizara ya Katiba wajadili uanzishaji haki binadamu katika biashara

Spread the loveMTANDAO wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), umefanya...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Sitta ang’ang’ana wanafunzi watibiwe bure, Serikali yagoma

Spread the loveMBUNGE wa Urambo, Margaret Sitta, ameishauri Serikali iweke utaratibu wanafunzi...

error: Content is protected !!