Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mafuriko yatikisa Kongwa, DC afunguka
Habari Mchanganyiko

Mafuriko yatikisa Kongwa, DC afunguka

Spread the love

MAFURIKO ya maji  mvua zinazoendelea kunyesha katika maeneo ya wilayani Kiteto mkoani Manyara, yamesababisha usumbufu kwa watumiaji wa barabara ya Morogoro-Dodoma, baada ya kufunga eneo la Kongwa mkoani Dodoma kwa saa kadhaa. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Akizungumza na MwanaHALISI Online kwa njia ya simu, leo tarehe 9 Januari 2024, Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mayeka Simon Mayeka amesema mafuriko hayo yalisababisha maji kujaa katika barabara eneo la Kongwa, na kusababisha magari na raia kushindwa kuitumia.

Mkuu wa Wilaya ya Kongwa, Mayeka Simon Mayeka.

Mayeka amesema kwa sasa maji hayo yamepungua na kwamba magari yameanza kuruhusiwa kutembea kwa awamu, huku akitaja athari za mafuriko hayo kuwa ni gari moja lililolazimisha kupita kabla ya kuruhusiwa na kudondoka. Hata hivyo, hakuna mtu aliyejeruhiwa au kupoteza maisha kufuatia mafuriko hayo.

“Ni sahihi kulikuwa na hali mbaya ya mafuriko toka asubuhi lakini sasa maji yameshapungua na tumeanza kuruhusu magari machache yapite kwa awamu. Athari kwa maana ya binadamu kupoteza maisha hakuna ila kuna gari lilijaribu kupita kabla ya askari kuruhusu lilidondoka,” amesema Mayeka na kuongeza:

“Chanzo cha mafuriko haya ni maji tunayopokea kutoka wilayani Kiteto ambako kunanyesha mvua sababu sisi huku mvua haikunyesha na sababu Kongwa iko chini maji yanajaa.”

Kuibuka wa taarifa hizi kumekuja baada ya baadhi ya wananchi kusambaza video zinazoonyesha barabara hiyo kujaa maji huku magari yakiwa kwenye mlolongo wa foleni baada ya kukwama kupita.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!