Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Askofu na mshauri wa Papa Francis ataka mapadre waruhusiwe kuoa
Habari Mchanganyiko

Askofu na mshauri wa Papa Francis ataka mapadre waruhusiwe kuoa

Askofu Charles Scicluna
Spread the love

Afisa mkuu wa Vatican ambaye pia ni mshauri wa Papa Francis, Askofu Mkuu Charles Scicluna amesema ipo haja ya Kanisa Katoliki kutathmini upya suala la mapdre kuoa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Charles Scicluna ambaye ni Askofu Mkuu wa Malta ametoa ushauri huo katika mahojiano yaliyochapishwa jana Jumapili na gazeti la Times of Malta.

Alisema: “Ni mara ya kwanza ninayasema haya hadharani na huenda yataonekana kuwa ya uzushi kwa baadhi ya watu.”

Askofu Scicluna, anayejulikana zaidi kwa uchunguzi wake wa uhalifu wa unyanyasaji wa kijinsia, alibainisha kuwa makasisi waliruhusiwa kuoa katika milenia ya kwanza ya historia ya Kanisa na kwamba ndoa inaruhusiwa leo katika ibada ya Mashariki ya Kanisa Katoliki.

“Kama ningelikuwa na uwezo, ningerekebisha masharti ya kuwataka makasisi kuwa waseja,” alisema na kuongeza kuwa;

“Uzoefu umenionyesha kuwa hili ni jambo tunalohitaji kufikiriwa kwa uzito.”

Askofu Mkuu Scicluna, 64, alisema Kanisa “limepoteza makasisi wengi wakuu kwa sababu walichagua ndoa”.

Alisema kuna mahali kwa useja katika Kanisa lakini pia ilibidi kuzingatia kwamba kasisi wakati mwingine wanapata hisia ya mapenzi.

“Hilo linapotokea anapaswa kuchagua kati ndoa na ukuhani na baadhi ya makuhani katika juhudi za kukabiliana na uamuzi huo wanaingia kisiri katika mahusiano ya kimapenzi”.

Mjadala kuhusu iwapo makasisi wa Kikatoliki waruhusiwe kuoa umekuwepo kwa karne nyingi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!