Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kiongozi kundi linalopinga wahamiaji Afrika Kusini akamatatwa
Kimataifa

Kiongozi kundi linalopinga wahamiaji Afrika Kusini akamatatwa

Spread the love

 

KIONGOZI nchini Afrika Kusini wa kundi linalopinga wahamiaji, amekamatwa siku ya Alhamisi tarehe 24 machi 2022 vyombo vya Habari nchini humo vinaripoti.

Nhlanhla Lux Dlamini mwenye umri wa miaka 33 ,ameripotiwa kuzuiliwa katika kituo cha Polisi katika mji mkuu wa kibiashara wa Johannesburg.

Hata hivyo sababu za kukamatwa kwake bado hazijabainika.

Kundi lake linalofahamika kwa jina la Operation Dudula ,limekuwa likifanya kampeni dhidi ya Raia wa kigeni wasio na vibali nchini.

Aidha uungwaji mkono wa kundi hilo, umekuwa ukiongezeka miongoni mwa jamii ya Waafrika Kusini wanaohisi kutengwa.

Kuna wasiwasi kwamba kampeni zake ,zinaweza kusababisha kuzuka kwa ghasia za chuki dhidi ya wageni nchini

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!