Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Japan yamuaga Shinzo Abe jijini Tokyo
Kimataifa

Japan yamuaga Shinzo Abe jijini Tokyo

Gari lililobeba mwili wa Shinzo Abe, likiwa nje ya Hekalu la Zojoji
Spread the love

WAOMBOLEZAJI wamepanga mistari kwenye barabara za mji mkuu wa Japan – Tokyo kumuaga aliyekuwa waziri mkuu wa nchi hiyo aliyeuawa Shinzo Abe.  Inaripoti Mitandao ya Kimataifa… (endelea).

Gari lililobeba mwili wake lilipitishwa katika maeneo muhimu ya kisiasa baada ya kufanyika ibada ya faragha. Hafla hiyo ilifanywa katika hekalu la Zojoji mjini Tokyo na kuhudhuriwa na ndugu, jamaa na marafiki wa karibu.

Pia mwili wake ulipitishwa katika majengo ya bunge, ofisi ya waziri mkuu na makao makuu ya chama chake cha Liberal Democratic.

Waziri mkuu huyo wa zamani aliyehudumu kwa muda mrefu zaidi nchini humo, aliuawa kwa risasi Ijumaa tarehe 8 Julai, 2022 wakati akifanya kampeni katika mji wa magharibi wa Nara. Tukio hilo liliishtua Japan na kulaaniwa na jamii ya kimataifa.

Mshukiwa wa mauaji hayi, Tetsuya Yamagami mwenye umri wa miaka 41, yuko kizuizini na amewaambia polisi alimlenga Abe kwa sababu aliamini mwanasiasa huyo alikuwa na mafungamano na kundi moja alilolichukia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!