Friday , 17 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Watano wa familia moja wafa ajali iliyoua wanane Kagera
Habari Mchanganyiko

Watano wa familia moja wafa ajali iliyoua wanane Kagera

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, William Mwampaghale
Spread the love

 

WATU watano wa familia moja wamefariki dunia katika ajali iliyosababisha vifo vya watu wanane baada ya magari mawili kugongana uso kwa uso katika barabara kuu ya kutoka Lusahunga kwenda Nyakahura wilayani Biharamulo Mkoa wa Kagera. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kagera … (endelea).

Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kagera, William Mwampaghale, ajali hiyo imetokea usiku wa leo Jumanne tarehe 12 Julai, 2022 ikihusisha gari aina ya Mercedez Benz na lori aina ya Toyota Probox.

Kamanda Mwampaghale ametaja ndugu wa familia moja waliofariki kuwa ni Jesca Ntahimula (45), Magreth Kimuna (14), Adidas Sekanabo (12), Zabloni (6) na Vedastina Sekanabo (8) wakazi wa Nyamalagala.

Wengine waliofariki kwenye ajali hiyo ni dereva wa Mercedes Benz, Vicent Gakuba (52) raia wa Rwanda, mkazi wa Nyamata Rugesela EAST Province, Nyawenda Bisalo (35) na Majaliwa Maige (32), wakazi wa Kikoma.

Kamanda huyo amesemaMiili ya marehemu hao imehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhia maiti Kituo cha Afya Nyakanazi.

Kamanda huyo amesema uchunguzi wa awlai umebainia chanzo cha ajali hiyo ni uzembe wa dreva wa lori aliyehama kutoka upande wake na kuendesha gari upande ambao sio wake kitendo kilichosababisha kugongana uso kwa uso kwa magari hayo.

Amesema dreva wa lori, Vicent Gakuba alitoroka baada ya ajali hiyo lakini polisi walifanikiwa kumkamata baada ya muda mfupi eneo la Rusumo akijaribu kutoroka kwenda Rwanda kwa kutumia lori.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Udhibiti wa serikali wakera asasi za kiraia

Spread the loveBaadhi ya wadau wa demokrasia na viongozi wa asasi za...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Nape aomba bajeti ‘kiduchu’ kwa mwaka 2024/25

Spread the loveWaziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Seneta: Wanasiasa hawasaidii mchakato wa Katiba mpya

Spread the loveSeneta wa jimbo la Busia, nchini Kenya, Okiya Okoiti Andrew...

Habari Mchanganyiko

Wananchi washauriwa kuongeza uelewa wa kujikinga na majanga

Spread the love WITO umetolewa kwa wananchi kuongeza uelewa na utayari kabla...

error: Content is protected !!