Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano
Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the love

JESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada ya kundi la wanamgambo wa kiislamu la Hamas, kudaiwa kukiuka makubaliano ya kusitisha mapigano, pamoja na kuwaacha huru mateka wote wa taifa hilo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kwa mujibu wa mtandao wa BBC Swahili, mashambulizi hayo ya Israel yameanza baada ya wanamgambo wa Hamas kuwafyatulia risasi wanajeshi wake, pamoja na kurusha roketi angani.

Waziri Mkuu wa Israel, Benjamin Netanyahu, amedai Hamas haijawaacha huur mateka wanawake kama walivokubaliana, badala yake wameanzisha mashambulizi asubuhi ya leo Ijumaa.

Jeshi la Israel na Hamas, walikubali kusitisha mapigano kwa muda, ili kutoa nafasi ya mateka wa pande zote mbili, kuachwa huru.

Hadi sasa Jeshi la Israel linasambaza vipeperushi vya onyo kwa wapalestina waishio kusini mwa Gaza, ikiwataka waondoke katika eneo hilo mara moja, kwa kuwa eneo hilo ni hatari kwa ajili ya mapigano.

Mtandao wa Aljazeera umeripoti kuwa, tangu Israel ianzishe mashambulizi hayo, watu zaidi ya 15 wamefariki dunia.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Antonio Guterres, amelaani mapigano kuanza upya, huku akitaka mpango wa kuyasitisha kwa muda ujadiliwe upya na pande zote mbili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!