Thursday , 9 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Genge la matapeli latua Chamwino, wananchi watahadharishwa
Habari Mchanganyiko

Genge la matapeli latua Chamwino, wananchi watahadharishwa

Spread the love

MTENDAJI wa Kijiji cha Huzi Kata ya Huzi Wilayani Chamwino mkoani Dodoma, Sospeter Ngalongwa amewataadharisha baadhi ya watu wanaoingia kijijini hapo kununua ardhi bila kupitia ofisi za viongozi kuwa wataangukia mikononi mwa kikundi cha  matapeli na kupata hasara itakayosababisha migogoro isiyokuwa na sababu. Anaandika Danson Kaijage, Dodoma (endelea).

Kiongozi huyo ametoa rai hiyo leo tarehe 15 Agosti 2023 baada ya kutokea wimbi la madalali katika kijiji hicho ambao wanajifanya wana maeneo wanayoyamiliki na kutaka kuyauza wakati maeneo hayo siyo ya kwao.

Amesema jambo hilolinaweza kusababisha mgogoro na machafuko.

Mmoja wa wasimamizi ya mashamba ambayo yamevamiwa na matapeli, Ndama Maduka akionesha shamba hilo analolimiki.

Akizungumzia malalamiko ambayo yanatolewa na baadhi ya wananchi kwa kuwepo kwa kundi hicho, Mtendaji huyo amesema kuna kikundi cha watu wanne ambao wanapita kwenye maeneo ya watu na kujiwekea mipaka na kujifanya kuwa ni maeneo yao jambo ambalo ni uongo.

Mmoja wa wananchi wa kijiji cha Huzi  ambao wamekumbana na adha ya matepeli waliotaka kuuza eneo lake ni mzee Mkhani Makuda ambaye amesema alishangazwa na baadhi ya watu ambao walianza kujigawia ardhi kwa madai kuwa wao ni wamiliki halali jambo ambalo ni udanganyifu.

“Walikuja vijana hapa wakiwa na wateja wakaanza kujigawia maeneo ambayo mimi (Maduka) nayamiliki wakidai kuwa wao ni wamiliki ya maeneo hayo, wakati nilianza kumiliki maeneo hayo zaidi ya miaka nane iliyopita nikiwa naendesha shughuli za kilimo na ufugaji kwa muda huo na nina nyaraka zote za umiliki.

“Baada ya kutokea hali hiyo nilitoa taarifa kwenye ofisi za kijiji na baada ya vijana hao kujua nimeshatoa taarifa kwa uongozi na kuonesha nyaraka za umiliki, walianza kutafuta njia nyingine ya kuuziana kienyeji jambo ambalo mpaka sasa hawajafanikiwa kufanya biashara kutokana kutokuwa na nyaraka yoyote ya mauziano,” ameeleza Mzee Maduka.

Kwa upande wake Ndama Maduka amesema kuwa madalali hao wasipothibitiwa ni wazi kuwa wanaweza kusababisha usumbufu kwa wananchi.

Hata hivyo, Maduu amesema viongozi wanatakiwa kuingilia kati tatizo hilo kwa haraka kabla ya hali haijawa mbaya.

Kwa upande wake Edward Mdowe ambaye anatuhumiwa na baadhi ya wananchi kwa maelezo kuwa anaongoza kikundi hicho cha matapeli alipoulizwa juu ya tuhuma hizo alikana kuhusika na badala yake alikata aulizwe kamishna wa ardhi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali yapunguza kodi ya makampuni kwa 20%

Spread the loveSERIKALI imepunguza kodi ya makampuni kwa asilimia 20, kutoka asilimia...

Habari Mchanganyiko

Mradi uliotaka kumng’oa madarakani Dk. Mpango waanza majaribio

Spread the loveMRADI wa maji wa Mwanga-Same-Korogwe, ambao Makamu wa Rais, Dk....

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Madiwani Msalala wampa tano DED kwa kuongeza mapato

Spread the loveMKURUGENZI wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala, mkoani Shinyanga, Khamis...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kimbunga Hidaya chaua 5, kaya 7,027 zikikosa makazi

Spread the loveSERIKALI imetoa tathmini ya athari za kimbunga Hidaya, kilichotokea tarehe...

error: Content is protected !!