DIEUDONNÉ Murengerantwari anatuhumiwa na wizara ya sheria ya Burundi kwa madai ya kuhujumu utendaji wa uchumi wa taifa, ufisadi na ufujaji wa mali ya umma. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea)
Licha ya tuhuma hizo, kiongozi huyo wa zamani hajajibu madai hayo.
Siku ya Jumapili, Rais wa Burundi, Évariste Ndayishimiye alimfuta kazi Murengerantwari na nafasi yake kuchukuliwa na Édouard Normand Bigendako.
Murengerantwari alikuwa ameteuliwa kuongoza benki kuu ya Burundi kwa miaka mitano kuanzia Agosti mwaka jana.
Kwa mujibu wa mwanasheria mkuu wa Burundi, Leonard Manirakiza uchunguzi zaidi kuhusu madai hayo ya ufisadi dhidi ya kiongozi huyo unaendelea.
Aidha, taarifa ya mwanasheria huyo mkuu wa Burundi inasema gavana huyo wa zamani wa benki kuu kwa sasa anashughulikiwa kwa mujibu wa sheria wakati akiendelea kuzuiliwa.
Leave a comment