Monday , 11 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Gavana wa benki kuu Burundi akamatwa kwa ufisadi
Kimataifa

Gavana wa benki kuu Burundi akamatwa kwa ufisadi

Spread the love

DIEUDONNÉ Murengerantwari anatuhumiwa na wizara ya sheria ya Burundi kwa madai ya kuhujumu utendaji wa uchumi wa taifa, ufisadi na ufujaji wa mali ya umma. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea)

Licha ya tuhuma hizo, kiongozi huyo wa zamani hajajibu madai hayo.

Siku ya Jumapili, Rais wa Burundi, Évariste Ndayishimiye alimfuta kazi Murengerantwari na nafasi yake kuchukuliwa na Édouard Normand Bigendako.

Murengerantwari alikuwa ameteuliwa kuongoza benki kuu ya Burundi kwa miaka mitano kuanzia Agosti mwaka jana.

Kwa mujibu wa mwanasheria mkuu wa Burundi, Leonard Manirakiza uchunguzi zaidi kuhusu madai hayo ya ufisadi dhidi ya kiongozi huyo unaendelea.

Aidha, taarifa ya mwanasheria huyo mkuu wa Burundi inasema gavana huyo wa zamani wa benki kuu kwa sasa anashughulikiwa kwa mujibu wa sheria wakati akiendelea kuzuiliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Sakata la uhamiaji Rwanda lamng’oa waziri Uingereza

Spread the loveWaziri wa Uhamiaji wa Uingereza, Robert Jenrick amejiuzulu baada ya...

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

error: Content is protected !!