Saturday , 11 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa El Chapo aomba kurejeshwa Mexico
Kimataifa

El Chapo aomba kurejeshwa Mexico

Joaquin ‘El Chapo’ Guzman
Spread the love

 

RAIS wa Mexico, Andres Manuel Lopez Obrador amesema atazingatia ombi la mlanguzi wa dawa za kulevya Joaquin ‘El Chapo’ Guzman, anayetumikia kifungo kurejea Mexico kutoka Marekani kumalizia kifungo chake kwa misingi ya kibinadamu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mwanzilishi wa genge la ulanguzi la Sinaloa ameomba msaada kwa Rais Obrador, kutokana na madai ya mateso ya kisaikolojia ambayo Guzman, anasema anateseka katika gereza la Marekani.

Rais Obrado aliwaambia wanahabari kwamba wanapitia maombi ya El Chapo. Haikuwa wazi kama Mexico ilikuwa na uwezo wa kukubaliana na ombi hilo.

Mwaka 2019, Mahakama ya serikali kuu mjini Brooklyn nchini Marekani ilimhukumu kifungo cha maisha jela El Chapo baada ya kupatikana na hatia ya kufanya biashara hiyo haramu iliyosababisha vifo vya watu wengi na kuingiza nchini Marekani tani nyingi za dawa ya kulevya.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!