Monday , 6 May 2024
Home Habari Mchanganyiko ASA yaongeza uzalishaji mbegu kufikia tani 3,500
Habari Mchanganyiko

ASA yaongeza uzalishaji mbegu kufikia tani 3,500

Spread the love

WAKALA wa Mbegu za Kilimo nchini (ASA), umesema uzalishaji mbegu imeongezeka kutoka tani 500 hadi kufikia 3,500. Anaripoti Mwandishi Wetu, Tabora…(endelea).

Ongezeko hilo limetajwa leo Jumatano na Mtendaji Mkuu wa ASA Dk. Sophia Kashenge, akizungumza uwekezaji katika sekta hiyo uliofanywa na Rais Dk. Samia Suluhu Hassan, tangu alivyoingia madarakani miaka miwili na nusu iliyopita.

“Tunampongeza sana Rais Samia kwa kuongeza bajeti ya ASA iliyotuwezesha kuongeza uzalishaji mbegu kwa kiasi kikubwa,” amesema Dk. Kashenge.

Dk. Kashenge amesema ongezeko hilo linawasaidia wakulima Kupata mbegu bora kwa bei nafuu na kwa uhakika.


Amesema idadi ya mashamba ya ASA imeongezeka kutoka nane hadi 16, yaliyoko Tanzania Bara, ambayo kwa sasa yanayotumika ni asilimia 90.

Dk. Kashenge amesema uwekezaji wa miundombinu Katima shamba la mbegu lililoko eneo la Kilimo, wilayani Nzega, Mkoa wa Tabora, utazalisha mbegu mara mbili mwaka ujao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari Mchanganyiko

Tanzania  yasisitiza kuwa Kituo Kikuu cha Uchimbaji Madini Afrika

Spread the loveTanzania imeendelea kusisitiza adhma yake ya kuwa kituo kikuu cha...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!