Monday , 11 December 2023
Home Kitengo Habari Kimataifa Uingereza yatahadharisha raia wake Uganda
Kimataifa

Uingereza yatahadharisha raia wake Uganda

Spread the love

Serikali ya Uingereza imetoa tahadhari kwa raia wake wajiepushe kuitembelea mbuga mashuhuri ya wanyama nchini Uganda ambako watalii wawili, akiwemo raia mmoja wa Uingereza, wameuawa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa …(endelea).

Maafisa wa polisi na wa mbuga ya wanyama wamesema watu hao watatu walishambuliwa jana Jumanne na watu waliokuwa na bunduki wakati walipokuwa wakifanya safari katika mbuga ya kitaifa ya Malkia Elizabeth kusini magharibi mwa Uganda na gari yao kutiwa moto.

Shirika la Huduma za Wanyamapori la Uganda limewatambua wahanga wengine wawili kama mtalii wa Afrika Kusini na muongozaji safari wa Uganda.

Polisi wamelinyooshea kidole cha lawama kundi la Allied Democratic Forces (ADF) kwa shambulizi hilo.

Msemaji wa polisi, Fred Enanga amesema vikosi vyao vya pamoja vilichukua hatua mara tu baada ya kupokea taarifa na wanawasaka washukiwa waasi wa kundi la ADF.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Kimataifa

Sakata la uhamiaji Rwanda lamng’oa waziri Uingereza

Spread the loveWaziri wa Uhamiaji wa Uingereza, Robert Jenrick amejiuzulu baada ya...

Kimataifa

Muandamanaji ajichoma moto akipinga vita Palestina, Israel

Spread the loveMUANDAMANAJI moja ambaye hajafahamika jina, yuko mahututi hospitalini akitetea uhai...

Kimataifa

Urusi kuongeza wanajeshi ikijihami dhidi ya NATO

Spread the loveSERIKALI ya Urusi iko katika mpango wa kuongeza wanajeshi wake,...

Kimataifa

Israel yarejesha mashambulizi Gaza ikilaumu Hamas kukiuka makubaliano

Spread the loveJESHI la Israel, limerejesha mashambulizi katika ukanda wa Gaza, baada...

error: Content is protected !!