Thursday , 9 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya Wanasayansi wagundua teknolojia ya kunyofoa VVU kutoka kwenye seli
AfyaTangulizi

Wanasayansi wagundua teknolojia ya kunyofoa VVU kutoka kwenye seli

Spread the love

TIMU ya wanasayansi kutoka Chuo Kikuu cha Amsterdam cha nchini Uholanzi imesema imefanikiwa kuondoa Virusi Vya Ukimwi (VVU) kutoka kwa chembechembe seli zilizoambukizwa kwa kutumia teknolojia ya uhariri wa jeni ya Crispr iliyoshinda Tuzo ya Nobel. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Teknolojia hiyo ambayo inafanya kazi kama mkasi, ndani ya molekuli, hukata DNA zilizoathiriwa ili ziweze kuondolewa.

Matumaini hayo yanathibitisha kuwa wanasayansi hao wanaweza kuondoa virusi mwilini, ingawa kazi nyingi zaidi inahitajika ili kuangalia iwapo njia hiyo itakuwa salama na yenye ufanisi.

Dawa zilizopo za VVU zinaweza kuzuia virusi lakini sio kuviondoa.

Muhktasari wa matokeo ya teknolojia hiyo umewasilishwa na timu ya Chuo Kikuu cha Amsterdam kutoka Uholanzi katika mkutano wa matibabu wiki hii.

Timu hiyo imesisitiza kazi yao inabaki kuwa uthibitisho wa kinadharia na sio tiba ya VVU kwa sasa.

Naye Dk. James Dixon ambaye ni Profesa msaidizi wa teknolojia ya seli shina na tiba ya jeni katika Chuo Kikuu cha Nottingham nchini Uingereza ameunga mkono matokeoya teknolojia hiyi na kusema kuwa matokeo kamili bado yanahitaji kuchunguzwa.

“Kazi zaidi itahitajika ili kuonyesha matokeo chanya katika majaribio haya ya seli yanavyoweza kutokea katika mwili mzima kwa tiba ya siku zijazo,” alisema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Lissu, Halima Mdee hapatoshi

Spread the loveVITA ya maneno kati ya Makamu Mwenyekiti wa Chama cha...

Habari za SiasaTangulizi

Bashiru Ally aivaa serikali kukalia vibali vya wahadhiri

Spread the loveMBUNGE wa kuteuliwa, Dk. Bashiru Ally amesema vikwazo vinavyoendekezwa na...

Habari za SiasaTangulizi

Bunge lamkaba koo Mo Dewji kwa kutelekeza viwanda vya chai

Spread the loveSERIKALI inakusudia kumuweka kikaangoni Mkurugenzi wa Kampuni ya Mohammed Enterprises...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

error: Content is protected !!