Mbunge wa viti maalumu Zainab Katimba amekabidhi mitungi ya gesi kwa vikundi vya wanawake wajasiriamali katika kata ya Mwandiga halmashauri ya Kigoma mkoani Kigoma ikiwa ni sehemu ya kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluh Hassan katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia. Anaripoti Faki Ubwa… (endelea).
Akizungumza baada ya kukabidhi mitungi hiyo Katimba amempongeza Rais Samia kwa kuhamasisha matumizi ya nishati safi nchini na kusisitiza kuwa hatua hiyo si tu itasadia kutunza mazingira lakini pia ni sehemu ya kuwahepusha wananchi na madhara yatokanayo na matumizi ya kuni na mkaa.
Mbunge huyo amewataka wanufaika wa mitungi hiyo kuwa mabolozi katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi kwenye maeneo yao ili dhamira ya Rais Samia iweze kutimia.
”Binafsi nimekuwa nikigawa mitungi hii kwa wanawake na leo nimekabidhi mitungi hamsini ikiwa ni sehemu ya mitungi miambili ambayo nimegawa kiu yangu ni kuona jamii inaondokana na matumizi ya nishati ya mkaa na kuni kama ambavyo rais wetu amekuwa akihamasisha” alisema Katimba.
Baadhi ya wanufaika wa mitungi hiyo wamempongeza Katimba kwa juhudi zake katika kuyakwamua makundi ya wanawake na kumtaja kama kiongozi mwanamke ambaye amekuwa begakwabega na wanawake wenzake mkoani humo.
Wanawake hao wamesema mitungi hiyo itawasaidia kufanya shughuli zao kwa urahisi na kuwawezesha watoto wao kusoma vizuri kwani hapo awali wamekuwa wakilazimika kuwatuma kutafuta kuni badala ya kwenda shuleni kuasoma.
” Hapo awali tumekuwa tukipata shida sana yaani mtu unatumia kuni hadi ule moshi unakufanya macho yawe mekundu ” alisema mmoja wawanufaika hao.
Katika hatua nyingine mbunge huyo amekabidhi mashuka katika kituo cha afya cha Mwandiga na zahanati ya Kiganza.
Katimba anaendelea na ziara yake inayolenga kuyafikia makundi mbalimbali ya wanawake mkoani Kigoma.
Leave a comment