Friday , 10 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Gavana wa benki kuu Burundi akamatwa kwa ufisadi
Kimataifa

Gavana wa benki kuu Burundi akamatwa kwa ufisadi

Spread the love

DIEUDONNÉ Murengerantwari anatuhumiwa na wizara ya sheria ya Burundi kwa madai ya kuhujumu utendaji wa uchumi wa taifa, ufisadi na ufujaji wa mali ya umma. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea)

Licha ya tuhuma hizo, kiongozi huyo wa zamani hajajibu madai hayo.

Siku ya Jumapili, Rais wa Burundi, Évariste Ndayishimiye alimfuta kazi Murengerantwari na nafasi yake kuchukuliwa na Édouard Normand Bigendako.

Murengerantwari alikuwa ameteuliwa kuongoza benki kuu ya Burundi kwa miaka mitano kuanzia Agosti mwaka jana.

Kwa mujibu wa mwanasheria mkuu wa Burundi, Leonard Manirakiza uchunguzi zaidi kuhusu madai hayo ya ufisadi dhidi ya kiongozi huyo unaendelea.

Aidha, taarifa ya mwanasheria huyo mkuu wa Burundi inasema gavana huyo wa zamani wa benki kuu kwa sasa anashughulikiwa kwa mujibu wa sheria wakati akiendelea kuzuiliwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Israel yatia shubiri Gaza wakisherehekea Hamas kusitisha mapigano

Spread the loveWAKATI kundi la Hamas huko Gaza likitangaza kuridhia pendekezo lao...

KimataifaMakala & Uchambuzi

Mbivu, mbichi urais wa Ramaphosa mwezi huu

Spread the loveMWISHONI mwa mwezi huu, raia wa Afrika Kusini watapiga kura...

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!