Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Afrika kusini waandamana kushinikiza serikali kumaliza tatizo la umeme
Kimataifa

Afrika kusini waandamana kushinikiza serikali kumaliza tatizo la umeme

Spread the love

 

MAMIA ya wafuasi wa Chama cha upinzani nchini Afrika Kusini – Democratic Alliance wameandamana jana tarehe 25 Januari 2023 kupinga kukatika kwa umeme kunakoendelea hali ambayo inazorotesha uchumi wa nchi hiyo iliyoendelea zaidi barani Afrika. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Afrika Kusini imeghubikwa na tatizo la nishati kwa zaidi ya muongo mmoja, lakini tatizo hilo limeongekeza zaidi mwaka huu, huku nchi hiyo ikikabiliwa na ukosefu wa umeme kila siku – wakati mwingine kwa muda wa saa 10 kwa siku.

Eskom – shirika la umeme la serikali lenye madeni, linakabiliwa na mitambo ya makaa ya mawe iliyochakaa ambayo inadaiwa kuharibika mara kwa mara.

Rushwa na hujuma pia zimelidhoofisha shirika hilo kwa kiasi kikubwa.

Kutokana na hali hiyo, Mkurugenzi Mtendaji, Andre de Ruyter wa shirika hilo anatarajiwa kuacha kazi mwishoni mwa Machi.

Mamia ya waandamanaji walikusanyika nje ya makao makuu ya chama tawala cha African National Congress, wakiilaumu serikali kwa kushindwa kutatua tatizo la umeme.

Mapema wiki hii, Rais Cyril Ramaphosa alisema serikali inaangalia suala la kuingiza umeme kutoka nje, lakini ameonya tatizo hilo haliwezi kutatuliwa kwa siku moja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!