JESHI la Polisi nchini Tanzania limesema hali ya ulinzi na usalama wa nchi ni shwari kwani limeendelea kudhibiti matukio makubwa yanayoweza kuleta hofu kwa wananchi. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).
Taarifa iliyotolewa leo Alhamisi tarehe 26 Januari kwa vyombo vya habari, Na Msemaji wa Jeshi la Polisi Tanzania, SACP David Misime, imekuja siku moja baada ya Ubalozi wa Marekani kutoa tahathari kwa watu wake juu ya uwezekano wa kutokea uhalifu wa kigaidi maeneo yanayopendwa kutembelewa na watu wengi.
Jeshi la polisi limesema lilianza kufuatilia taarifa hizo na kuwataka wananchi waendelee kuwa watulivu na kuendelea na shughuli zao kama kawaida.
“Jeshi la polisi Tanzania tulianza kuifanyia kazi taarifa hiyo kwa kina toka ilipoanza kusambaa katika vyombo vya habari… itakapobainika jambo lenye kutia shaka au atakapoonekana mtu mqenye kutia shaka kutokana na mienendo yao, basi taarifa hizo ziripotiwe kwa haraka ili kufanyiwa kazi, ” imeeleza taarifa hiyo.
Taarifa hiyo imeeleza mikakati yake ya kuhakikisha wanabaini na kuzuia ubalifu kwa kiwango kikubwa zaidi kwa mwaka 2023.
Ametaja mikakati hiyo kuwa ni pamoja kutoa elimu kwa umma ili kuongeza uelewa wa wananchi wa namna ya kushirikiana na jeshi la polisi kuzuia uhalifu kabla haujatokea.
“Kupitia ushirikiano wa wananchi utafiti unaonesha tutaweza kuwa na vyanzo vingi zaidi vya kupata taarifa nyingi zaidi za kuzuia,” amesema SACP Misime.
Leave a comment