RAIS wa Ukraine, Volodymyr Zelenskiy amesema anafanya mabadiliko ya maafisa wake wa ngazi ya juu na chini serikalini, kutokana na madai ya ufisadi yaliyoibuka nchini humo tangu Urusi iivamie nchi yake Februari mwaka jana. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Sakata hilo la ufisadi huenda likapunguza ari ya nchi za Magharibi kuisaidia serikali yake wakati ambapo kuna mvutano miongoni mwa mataifa ya Ulaya kuhusu suala la kupeleka vifaru chapa Leopard 2 kutoka Ujerumani kueleke Ukraine.
Ukraine inasema inavihitaji vifaru hivyo ili kukabiliana na jeshi la Urusi na kuyarudisha katika himaya yake maeneo yaliyotekwa.
Juzi tarehe 22 Januari, 2023, polisi wa kukabiliana na ufisadi nchini Ukraine walisema kwamba wanamshikilia naibu waziri wa miundombinu kwa madai ya kupokea rushwa ya dola 400,000 katika uagizaji wa jenereta kutoka nje ya nchi mwezi Septemba.
Utafiti mmoja wa gazeti pia uliituhumu wizara ya ulinzi kwa kulipa fedha kupita kiasi kwa ajili ya chakula cha wanajeshi. Ukraine ina historia ndefu ya ufisadi na utawala usio thabiti.
Leave a comment