Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kashfa ya ufisadi yaitafuna Ukraine katikati ya vita
Kimataifa

Kashfa ya ufisadi yaitafuna Ukraine katikati ya vita

Spread the love

 

RAIS wa Ukraine, Volodymyr Zelenskiy amesema anafanya mabadiliko ya maafisa wake wa ngazi ya juu na chini serikalini, kutokana na madai ya ufisadi yaliyoibuka nchini humo tangu Urusi iivamie nchi yake Februari mwaka jana. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Sakata hilo la ufisadi huenda likapunguza ari ya nchi za Magharibi kuisaidia serikali yake wakati ambapo kuna mvutano miongoni mwa mataifa ya Ulaya kuhusu suala la kupeleka vifaru chapa Leopard 2 kutoka Ujerumani kueleke Ukraine.

Ukraine inasema inavihitaji vifaru hivyo ili kukabiliana na jeshi la Urusi na kuyarudisha katika himaya yake maeneo yaliyotekwa.

Juzi tarehe 22 Januari, 2023, polisi wa kukabiliana na ufisadi nchini Ukraine walisema kwamba wanamshikilia naibu waziri wa miundombinu kwa madai ya kupokea rushwa ya dola 400,000 katika uagizaji wa jenereta kutoka nje ya nchi mwezi Septemba.

Utafiti mmoja wa gazeti pia uliituhumu wizara ya ulinzi kwa kulipa fedha kupita kiasi kwa ajili ya chakula cha wanajeshi. Ukraine ina historia ndefu ya ufisadi na utawala usio thabiti.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!