Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Kagame akana Rwanda kuchochea vita Congo DRC
Kimataifa

Rais Kagame akana Rwanda kuchochea vita Congo DRC

Spread the love

 

RAIS wa Rwanda, Paul Kagame, amedai kwamba Serikali yake haichochei mgogoro wa kivita unaoendelea mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na BBC Swahili, Rais Kagame ametoa kauli hiyo jana Jumatano, akiwa nchini Marekani, alipoulizwa na waandishi wa habari kuhudu hatua ambazo Serikali yake inazichukua, kukomesha mauaji ya raia yanayoendelea kutokea katika vita hiyo.

Swali hilo limekuja baada ya Rais wa DRC, Felix Tshisekedi, katika mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Antony Blinken, uliofanyika Jumanne, kudai vita inayoendelea nchini mwake inachochea kwa siri na Rwanda.

“Tatizo halikuanzishwa na Rwanda na sio tatizo la Rwanda, ni tatizo la Congo,” Rais Kagame alikanusha madai hayo.

Kwa muda mrefu Serikali ya Rwanda imekabiliwa na tuhuma za kuwaunga mkono ikiwemo kuwapa silaha waasi wanaopigana na vikosi vya ulinzi na usalama vya DRC.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!