Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Kagame akana Rwanda kuchochea vita Congo DRC
Kimataifa

Rais Kagame akana Rwanda kuchochea vita Congo DRC

Spread the love

 

RAIS wa Rwanda, Paul Kagame, amedai kwamba Serikali yake haichochei mgogoro wa kivita unaoendelea mashariki mwa nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na BBC Swahili, Rais Kagame ametoa kauli hiyo jana Jumatano, akiwa nchini Marekani, alipoulizwa na waandishi wa habari kuhudu hatua ambazo Serikali yake inazichukua, kukomesha mauaji ya raia yanayoendelea kutokea katika vita hiyo.

Swali hilo limekuja baada ya Rais wa DRC, Felix Tshisekedi, katika mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika na Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Antony Blinken, uliofanyika Jumanne, kudai vita inayoendelea nchini mwake inachochea kwa siri na Rwanda.

“Tatizo halikuanzishwa na Rwanda na sio tatizo la Rwanda, ni tatizo la Congo,” Rais Kagame alikanusha madai hayo.

Kwa muda mrefu Serikali ya Rwanda imekabiliwa na tuhuma za kuwaunga mkono ikiwemo kuwapa silaha waasi wanaopigana na vikosi vya ulinzi na usalama vya DRC.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!