RAIS wa Marekani Joe Biden ameahidi kuimarisha uhusiano na mataifa ya Afrika, huku akitangaza kusudio la Serikali yake kutoa kiasi cha Dola 55 bilioni (Sh. 128.4 trilioni), kwa ajili ya kusaidia bara hilo kwenye masuala ya chakula na mabadiliko ya tabia ya nchi. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa…(endelea).
Kwa mujibu wa mtandao wa Reuters, Rais Biden alitoa ahadi hiyo jana Jumatano, katika hafla ya chakula cha jioni na viongozi wa mataifa ya Afrika, iliyofanyika katika Ikulu ya White House.
Nao mtandao wa BBC Swahili, leo Alhamisi, umeripoti kwamba kiongozi huyo wa Marekani, ametangaza makubaliano yenye lengo la kuimarisha uhusiano wa kibiashara kati ya taifa lake na nchi za Afrika, uliodorora kufuatia China kuongeza ushawishi wake barani humo.
Biden alisema mkataba mpya na eneo la Biashara Huria la Bara la Afrika, utazipa kampuni za Kimarekani uwezo wa kufikia watu bilioni 1.3 na soko lenye thamani ya dola trilioni 3.4.
Mkutano wa wakuu wa nchi za Afrika na Serikali ya Marekani, unafanyika kwa siku tatu, kuanzia Jumanne hadi Alhamisi, ambapo marais mbalimbali wamehudhuria akiwemo Rais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan. Rais wa Kenya, Dk. William Ruto. Rais wa Uganda, Yoweri Museveni na Rais wa Rwanda, Paul Kagame.
Leave a comment