Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Ufaransa kuwapiga msasa wanajeshi 2000 wa Ukraine
Kimataifa

Ufaransa kuwapiga msasa wanajeshi 2000 wa Ukraine

Spread the love

 

WAKATI vita kati ya Urusi na Ukraine ikiendelea kupamba moto, Taifa la Ufaransa limetangaza kuanza kuwapa mafunzo maalumu wanajeshi 2,000 wa Ukraine kwa wiki kadhaa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Hayo yameelezwa na Waziri wa Ulinzi, Sébastien Lecornu kwenye Gazeti la Le Parisien toleo la jana tarehe 16 Oktoba, 2022.

Hii ni mara ya kwanza kwa Ufaransa kujitolea kuratibu wa mafunzo ya kijeshi ya aina yake tangu kuanza kwa mgogoro wa kijeshi nchini Ukraine.

Ufaransa ilikuwa tayari imewapokea wapiganaji wa Ukraine ili kuwafundisha jinsi ya kutumia bunduki maarufu za Caesar, lakini wakati huu programu iliyotangazwa na Sébastien Lecornu ni ukubwa na ya tofauti.

Wanajeshi 2,000 watapokelewa nchini Ufaransa kwa mafunzo katika ngazi tatu: mafunzo ya jumla ya wapiganaji, vifaa na mafunzo kuhusu vifaa vinavyotolewa na Ufaransa.

Tangu kuanza kwa mzozo huo, nchi zingine mbali na Ufaransa zimepokea wanajeshi wa Ukraine kwa mafunzo katika nchi zao, hasa Uingereza.

Mafunzo ya vifaa yatahusu bunduki za Caesar, lakini pia makombora ya kulipua vifaru yaitwayo Milan, makombora ya kudungua ndege yaitwayo Mistral na hivi karibuni mfumo wa ulinzi wa makombora uitwao Crotale.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!