WAKATI vita kati ya Urusi na Ukraine ikiendelea kupamba moto, Taifa la Ufaransa limetangaza kuanza kuwapa mafunzo maalumu wanajeshi 2,000 wa Ukraine kwa wiki kadhaa. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).
Hayo yameelezwa na Waziri wa Ulinzi, Sébastien Lecornu kwenye Gazeti la Le Parisien toleo la jana tarehe 16 Oktoba, 2022.
Hii ni mara ya kwanza kwa Ufaransa kujitolea kuratibu wa mafunzo ya kijeshi ya aina yake tangu kuanza kwa mgogoro wa kijeshi nchini Ukraine.
Ufaransa ilikuwa tayari imewapokea wapiganaji wa Ukraine ili kuwafundisha jinsi ya kutumia bunduki maarufu za Caesar, lakini wakati huu programu iliyotangazwa na Sébastien Lecornu ni ukubwa na ya tofauti.
Wanajeshi 2,000 watapokelewa nchini Ufaransa kwa mafunzo katika ngazi tatu: mafunzo ya jumla ya wapiganaji, vifaa na mafunzo kuhusu vifaa vinavyotolewa na Ufaransa.
Tangu kuanza kwa mzozo huo, nchi zingine mbali na Ufaransa zimepokea wanajeshi wa Ukraine kwa mafunzo katika nchi zao, hasa Uingereza.
Mafunzo ya vifaa yatahusu bunduki za Caesar, lakini pia makombora ya kulipua vifaru yaitwayo Milan, makombora ya kudungua ndege yaitwayo Mistral na hivi karibuni mfumo wa ulinzi wa makombora uitwao Crotale.
Leave a comment