Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kongo wamtimua msemaji wa MONUSCO
Kimataifa

Kongo wamtimua msemaji wa MONUSCO

Spread the love

SERIKALI ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo imemtaka msemaji wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa nchini humo (MONUSCO), Mathias Gilman kuondoka haraka iwezekanavyo. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Serikali hiyo imesema msemaji huyo ametoa matamshi yasiyofaa yaliyochangia mvutano kati ya wananchi na MONUSCO.

Wiki iliyopita, watu 30 waliuawa wakati wa maandamano yaliyoibuka mashariki mwa nchi hiyo.

Miongoni mwa waliopoteza maisha ni walinda amani wa Umoja wa Mataifa na maofisa wa polisi.

Waandamanaji walilalamikia kile walichosema ni kushindwa kwa MONUSCO kuzuia mauaji yanayofanywa na makundi ya waasi.

Tarehe 31 Julai, 2022 watu watatu waliuawa baada ya walinda amani hao walipowafyatulia risasi katika kituo kimoja cha mpakani.

MONUSCO inakamilisha jukumu lake mwaka 2024 kwa mujibu wa mpango uliotangazwa mwaka jana, lakini serikali ya Kongo inataka iharakishe kuondoka kwake.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!