Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali kufuta ada kidato cha tano, sita
ElimuHabari za SiasaTangulizi

Serikali kufuta ada kidato cha tano, sita

Wanafunzi wa kidato cha sita walipokuwa wanafanya mtihani
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imetangaza kusudio la kufuta ada kwa wanafunzi wa kidato cha tano na sita, katika mwaka wa fedha ujao wa 2022/23. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo yamelezwa leo Jumanne, tarehe 14 Juni 2022, bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2022/23.

“Kwa sasa tuna takribani wanafunzi 90,825 wa kidato cha tano na 56,880 wa kidato cha sita. Mahitaji ya fedha ni takribani Sh. 10.3 bilioni. Ili kuwapunguzia gharama watoto hawa, napendekeza kufuta ada ya wanafunzi wa kidato cha tano na sita,” amesema Dk. Mwigulu.

Dk. Mwigulu amesema, kufuatia hatua hiyo, elimu bila malipo itaanza katika shule ya msingi hadi kidato cha tano na sita.

Aidha, Dk. Mwigulu amesema, Serikali inaangalia namna ya kusaidia wanafunzi wa vyuo vya kati, pindi hali ya uchumi wa nchi itakavyokuwa imetengemaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!