Wednesday , 24 April 2024
Home Kitengo Maisha Elimu Serikali kufuta ada kidato cha tano, sita
ElimuHabari za SiasaTangulizi

Serikali kufuta ada kidato cha tano, sita

Wanafunzi wa kidato cha sita walipokuwa wanafanya mtihani
Spread the love

 

SERIKALI ya Tanzania imetangaza kusudio la kufuta ada kwa wanafunzi wa kidato cha tano na sita, katika mwaka wa fedha ujao wa 2022/23. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam … (endelea).

Hayo yamelezwa leo Jumanne, tarehe 14 Juni 2022, bungeni jijini Dodoma na Waziri wa Fedha na Mipango, akiwasilisha makadirio ya mapato na matumizi ya Serikali kwa mwaka wa fedha wa 2022/23.

“Kwa sasa tuna takribani wanafunzi 90,825 wa kidato cha tano na 56,880 wa kidato cha sita. Mahitaji ya fedha ni takribani Sh. 10.3 bilioni. Ili kuwapunguzia gharama watoto hawa, napendekeza kufuta ada ya wanafunzi wa kidato cha tano na sita,” amesema Dk. Mwigulu.

Dk. Mwigulu amesema, kufuatia hatua hiyo, elimu bila malipo itaanza katika shule ya msingi hadi kidato cha tano na sita.

Aidha, Dk. Mwigulu amesema, Serikali inaangalia namna ya kusaidia wanafunzi wa vyuo vya kati, pindi hali ya uchumi wa nchi itakavyokuwa imetengemaa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!