Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri Mkuu Uingereza kikaangoni
Kimataifa

Waziri Mkuu Uingereza kikaangoni

Spread the love

Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson anajiandaa kubaki au kutoka ofisini baada ya kukamilika kwa matokeo ya uchunguzi wa sherehe zilizofanyika katika makazi yake na afisi yake ya Downing Street wakati nchi hiyo ilipokuwa imefungwa kwa ajili ya kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).

Nyaraka za matokeo hayo zitamsaidia kujua iwapo atafikia kikomo cha wiki kadhaa za sakata hilo ambalo limempaka matope mbele ya Waingereza au uongozi wake utafikia mwisho ghafla.

Ripoti zinaarifu kwamba Sue Gray anayeongoza uchunguzi huo, huenda akawasilisha ripoti yake kwa serikali hii leo tarehe 26 Januari, 2022.

Ofisi ya Johnson imeahidi kuchapisha matokeo ya uchunguzi huo na waziri mkuu huyo atalihutubia Bunge kuhusu matokeo hayo baada ya ripoti kuwasilishwa.

Ofisi ya Gray haikutoa tamko kwamba ni lini itatoa ripoti yake na serikali Uingereza imesema haijapokea ripoti yoyote kufikia asubuhi ya leo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!