Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Stendi ya daladala sabasaba kufumuliwa
Habari Mchanganyiko

Stendi ya daladala sabasaba kufumuliwa

Spread the love

 

MKURUGENZI wa Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru amesema wanatarajia kuifumua stendi ya daladala na soko la sabasaba iliyopo katikati ya jiji hilo na kuijenga upya. Anaripoti Danson Kaijage,  Dodoma … (endelea)

Hatua hiyo imelenga kuboresha mazingira ya jiji la Dodoma, maeneo ya masoko na stendi ya daladala.

Mafuru ametoa taarifa hiyo leo tarehe 26 Januari, 2022 katika kikao cha baraza la madiwani nijini Dodoma.

Amesema kuwa pamoja na kuwepo kwa changamoto ya masoko na stendi ya daladala, tayari wameanaza kukusanya maoni kutoka kwa wadau ili kuona namna ya kuboresha stendi hiyo, masoko ya sabasaba, majengo na makole.

Mkurugenzi wa Jiji la Dodoma, Joseph Mafuru

Amesema stendi ya sabasaba siyo stendi rasmi hivyo kunahitajika uboreshaji mkubwa kwa kufumua stendi pamoja sehemu za biashara.

“Mradi huo unatarajiwa kuanza kati ya Julai na Septemba kwa ufadhili wa Benki ya Dunia na mradi huo mkubwa utakamilika kwa miaka mitatu,” amesema Mafuru.

Katika hatua nyingine amesema jiji la Dodoma ni kati ya majiji ambayo yamepangwa kwa mpangilio mzuri hivyo utaratibu huo utaendelea kutekelezeka.

Aidha, Mafuru amewataka watu wanaoendeleza maeneo yao kufuata utaratibu wa kuomba vibali rasmi vya ujenzi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!