Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Waziri Mkuu Uingereza kikaangoni
Kimataifa

Waziri Mkuu Uingereza kikaangoni

Spread the love

Waziri Mkuu wa Uingereza, Boris Johnson anajiandaa kubaki au kutoka ofisini baada ya kukamilika kwa matokeo ya uchunguzi wa sherehe zilizofanyika katika makazi yake na afisi yake ya Downing Street wakati nchi hiyo ilipokuwa imefungwa kwa ajili ya kudhibiti maambukizi ya virusi vya corona. Anaripoti Mwandishi Wetu… (endelea).

Nyaraka za matokeo hayo zitamsaidia kujua iwapo atafikia kikomo cha wiki kadhaa za sakata hilo ambalo limempaka matope mbele ya Waingereza au uongozi wake utafikia mwisho ghafla.

Ripoti zinaarifu kwamba Sue Gray anayeongoza uchunguzi huo, huenda akawasilisha ripoti yake kwa serikali hii leo tarehe 26 Januari, 2022.

Ofisi ya Johnson imeahidi kuchapisha matokeo ya uchunguzi huo na waziri mkuu huyo atalihutubia Bunge kuhusu matokeo hayo baada ya ripoti kuwasilishwa.

Ofisi ya Gray haikutoa tamko kwamba ni lini itatoa ripoti yake na serikali Uingereza imesema haijapokea ripoti yoyote kufikia asubuhi ya leo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!