Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wafungwa 38 wafariki kwa ajali ya moto gerezani, 69 wajeruhiwa
Kimataifa

Wafungwa 38 wafariki kwa ajali ya moto gerezani, 69 wajeruhiwa

Spread the love

Takriban wafungwa 38 wamefariki dunia na wengine 69 kujeruhiwa katika ajali ya moto ulioteketeza gereza kuu la mji mkuu wa Burundi – Gitega mapema. Anaripoti Mwandishi Wetu.. (endelea)

Moto huo uliozuka mapema leo Jumanne tarehe 7 Disemba, 2021 bado haijabainika ni nini chanzo cha moto huo.

Kwa mujibu wa Makamu wa rais wa Burundi, Prosper Bazombanza ambaye alitembelea kituo hicho na hospitali ambapo wengi wa majeruhi wanatibiwa, amesema 12 kati ya waliofariki walikosa pumzi kwa kuzingirwa na moshi wakati 26 waliosalia walipata majeraha ya moto.

Amewaambia waandishi wa habari kuwa majeruhi 34 waliopata majeraha ya moto ya wastani na zaidi wamepelekwa hospitali huku wengine wakipatiwa matibabu katika eneo la gereza.

“Wafanyikazi wa afya wametuhakikishia kwamba watapona”, alisema. Ameongeza kuwa gharama za matibabu zitalipwa kikamilifu na serikali.

Hali mbaya ya usalama ilifanya iwe rahisi kwa moto huo kuenea haraka katika gereza hilo lenye uwezo wa kubeba watu 400 lakini sasa lilikuwa na wafungwa zaidi ya 1500. Kiwango kamili cha uharibifu kilikuwa bado hakijajulikana.

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!