Sunday , 5 May 2024
Home Gazeti Habari Rais Samia ateua DC, ahamisha 2
HabariTangulizi

Rais Samia ateua DC, ahamisha 2

Spread the love

RAIS wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan amemteua Dadi Horace Kolimba kuwa Mkuu wa Wilaya (DC) ya Karatu mkoani Arusha. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Uteuzi huo, umetangazwa leo Jumamosi, tarehe 4 Desemba 2021, na Jaffar Haniu, Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Kolimba anakwenda kuchukua nafasi ya Abbas Juma Kayanda ambaye amehamishiwa Wilaya ya Moshi, Mkoa wa Kilimanjaro.

Kayanda amekwenda kuchukua nafasi ya Said Mtanda ambaye Rais Samia amemhamishia Wilaya ya Arusha.

Mtanda amekwenda kujaza nafasi iliyokuwa wazi, kufuatilia aliyekuwa mkuu wa wilaya hiyo, Sophia Mjema, kuteuliwa na Rais Samia kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mbatia ambwaga Selasini, mahakama yaamuru alipwe fidia

Spread the loveMAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam, imemuamuru...

Habari za SiasaTangulizi

Mkulo afariki dunia, kuzikwa kesho Kilosa

Spread the loveALIYEKUWA Waziri wa Fedha na Mbunge wa Kilosa (CCM), Mustafa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Usafiri baharini wasitishwa kukwepa athari za kimbunga Hidaya

Spread the loveUSAFIRI wa baharini umesimamishwa kwa muda ili kukwepa athari za...

error: Content is protected !!