Thursday , 23 March 2023
Home Gazeti Habari Rais Samia: Machinga tuendelee kuvumiliana
HabariTangulizi

Rais Samia: Machinga tuendelee kuvumiliana

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa rai kwa wafanya biashara wadogo wadogo ‘machinga’ kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kwa kuwa kazi ya kuwaondoa barabarani ni kwa nia njema ya maendeleo yao wenyewe hapo baadae. Anaripoti Matilda Buguye… (endelea)

Pia amesema uamuzi wa Serikali unalenga kuwajengea mazingira na sasa inaendelea kukusanya fedha kwa ajili ya kuwajengea maeneo mazuri na yakudumu kwa ajili ya biashara zao. 

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 4 Disemba, 2021 katika hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka awamu ya pili, Mbagala rangi tatu jijini Dar es salaam.

Huku akiambatana na viongozi mbalimbali wa serikali katika hafla hiyo iliyopambwa na vikundi mbalimbali vya burudani ilivyoshuhudiwa na wananchi wa Mbagala walioweza kuhudhuria kwenye hafla hiyo.

Aidha, Rais Samia awakemea baadhi ya wananchi wasiokua na uzalendo ambao wanajihusisha na kuhujumu jitihada za utekelezaji wa mradi  huo wa ujenzi kwa kufanya vitendo vya wizi wa vifaa mbalimbali vinavyotumika.

Hivyo awaomba wananchi walio na uzalendo watakapogundua juu ya uhujumu wa aina yeyote juu ya ujenzi huo waseme na kutoa taarifa sehemu husika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari

Ugonjwa wa ajabu ulioua watano Bukoka ni Marburg

Spread the loveWAZIRI wa Afya, Ummy Mwalimu amesema ugonjwa wa ajabu uliosababisha...

AfyaHabariHabari

Ugonjwa wa ajabu wadaiwa kuua watano Kagera, Serikali yatoa tahadhari

Spread the loveJUMLA ya watu watano wanaidaiwa kufariki dunia  katika vijiji vya...

ElimuHabari

CBE yaanzisha Shahada 10 za Uzamili, CBE yajivunia wahitimu wanaoajirika

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimewataka wenye  kampuni na...

Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia ampandisha cheo RPC wa Dar

Spread the loveMKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, amesema...

error: Content is protected !!