Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari Rais Samia: Machinga tuendelee kuvumiliana
HabariTangulizi

Rais Samia: Machinga tuendelee kuvumiliana

Spread the love

RAIS Samia Suluhu Hassan ametoa rai kwa wafanya biashara wadogo wadogo ‘machinga’ kuwa wavumilivu katika kipindi hiki kwa kuwa kazi ya kuwaondoa barabarani ni kwa nia njema ya maendeleo yao wenyewe hapo baadae. Anaripoti Matilda Buguye… (endelea)

Pia amesema uamuzi wa Serikali unalenga kuwajengea mazingira na sasa inaendelea kukusanya fedha kwa ajili ya kuwajengea maeneo mazuri na yakudumu kwa ajili ya biashara zao. 

Rais Samia ametoa kauli hiyo leo tarehe 4 Disemba, 2021 katika hafla ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa miundombinu ya mabasi yaendayo haraka awamu ya pili, Mbagala rangi tatu jijini Dar es salaam.

Huku akiambatana na viongozi mbalimbali wa serikali katika hafla hiyo iliyopambwa na vikundi mbalimbali vya burudani ilivyoshuhudiwa na wananchi wa Mbagala walioweza kuhudhuria kwenye hafla hiyo.

Aidha, Rais Samia awakemea baadhi ya wananchi wasiokua na uzalendo ambao wanajihusisha na kuhujumu jitihada za utekelezaji wa mradi  huo wa ujenzi kwa kufanya vitendo vya wizi wa vifaa mbalimbali vinavyotumika.

Hivyo awaomba wananchi walio na uzalendo watakapogundua juu ya uhujumu wa aina yeyote juu ya ujenzi huo waseme na kutoa taarifa sehemu husika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

error: Content is protected !!