Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Wanafunzi wapigwa marufuku mavazi ya ‘Squid Game’
Kimataifa

Wanafunzi wapigwa marufuku mavazi ya ‘Squid Game’

Spread the love

 

SHULE tatu za msingi katika jimbo la New York nchini Marekani zimepiga marufuku mavazi ya ‘Halloween’ yanayofanana na yale yaliyovaliwa na washiriki wa tamthilia maarufu ya Netflix, Squid Game, kwa kuhofia kwamba yanaweza kuchochea vurugu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tamthilia hiyo ya kusisimua ya Korea Kusini inaeleza kuhusu hadithi ya watu wazima wanaoshindania zawadi ya pesa kwa kucheza michezo ya watoto, na ambao wako tayari kuhatarisha maisha yao ili kushinda.

Maudhui yake yanayoonekana kwenda kinyume na maadili kwa baadhi ya jamii yamesababisha shule kuwatumia barua pepe wazazi kuhusu ujumbe wa uchochezi uliomo kwenye tamthilia hiyo.

Shule hizo zimesema mavazi ya mchezo wa Squid katika hafla za shule hayatafaa.

Mkuu wa Shule ya Fayetteville ya New York, Dk. Craig Tice amesema muongozo wa shule hiyo umepiga marufuku mavazi ya Halloween yenye vitu vinavyoweza kufasiriwa kama silaha na vya kutisha.

Nchini Marekani, tamthilia hiyo imewekwa na mtandao wa Netflix kwenye darala la kuangaliwa na hadhira ya watu wazima hii ikimaanisha kwamba tammthili hiyo haitakiwi kutazamwa na watoto chini ya umri wa miaka 17.

Aidha, baadhi ya wazazi wanaripotiwa kutofurahishwa na marufuku hiyo ya mavazi iliyotolewa na shule hizo.

“Ni vazi tu. Jambo la msingi ni kutoruhusu watoto wako kutazama tamthilia hiyo,” amesema mwanamke mmoja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!