PAZIA la michuano ya Klabu Bingwa Ulaya limefunguliwa rasmi tarehe 14, 15 Septemba mwaka huu na kushuhudia mastaa namba moja duniani, Lionel Messi na Cristiano Ronaldo ambao wamezichea timu walizosajiliwa kwa mara ya kwanza, wakishindwa kuzipatia pointi tatu katika mechi za awali. Anaripoti Hunda Mintanga TUDARCo … (endelea).
Ronaldo ambaye amesajiliwa na Manchester United kutoka Juventus alishuhudia mashetani hao wekundu wakiangukia pua kwa bao 2-1 kutoka kwa vijana wa Young Boys (Uswiss) ilihali Messi ambaye amechomoka kutoka Barcelona kuelekea PSG ya Ufaransa jana tarehe 16 Septemba aliambulia sare ya 1-1 kutoka kwa Club Brugge (Ubelgiji).
Manchester United waliopo kundi F katika mchezo huo wa kwanza tarehe 14 Septemba, Ronaldo alifungua dimba kwa bao pekee kabla ya Young Boys kuondoka na ushindi.
Jana tarehe 15, PSG walio kundi A nao walibanwa mbavu licha ya kumchezesha Messi ambaye ni kipenzi cha wapenda soka wengi duniani.
Matokeo ya michezo mingine ni kwamba Manchester City wakiwa nyumbani Uingereza wamepata ushindi mnono wa bao 6-3 dhidi ya RB Leipzig, Atletico Madrid 0-0 FC Porto ya Ureno, Liverpool 3-2 AC Milan, Sporting 1-5 Ajax, Inter Milan wakiwa nyumbani pia walipoteza kwa kukubali kipigo cha goli moja kutoka kwa Real Madrid.
Leave a comment