Tuesday , 30 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Talban waua 20 ngome ya upinzani
Kimataifa

Talban waua 20 ngome ya upinzani

Spread the love

 

RAIA zaidi ya 20 wameuawa katika bonde la maajabu la Panjshir nchini Afghanistan katika mapigano baina ya Taliban na vikosi vya upinzani. Inaripoti Helena Mkonyi, TUDARCo kwa msaada wa Mitandao ya Kimataifa … (endelea)

Vyanzo vya habari vimeripoti, miongoni mwa waathirika wa tukio hilo ni muuzaji na baba wa watoto wawili Abdul Sami.

Wakati wa mapigano hayo, Sami hakutaka kuondoka katika eneo hilo la tukio huku akisema, yeye anamiliki duni na wala hana uhusiano wowote na mapigano hayo.

Lakini muuuzaji huyo, alikamatwa akituhumiwa kuuza kadi za simu kwa wapiganaji wa upinzani hali iliyosababisha kuuawa na mwili wake kutupwa karibu na nyumba yake.

Mashuhuda wa mwili huo walisema, mwili wa Sami ulionesha dalili zote za kuteswa kabla ya kifo chake.

Bonde hilo maarufu nchini humo la Panjshir, limekuwa kitovu cha upinzani Afghanistan chini ya kamanda wa upinzani Ahmad Shah Massoud, eneo hilo liliwafukuza vikosi vya Soviet na Taliban.

Bonde hilo limezungukwa na milima ambayo inawawia ngumu kwa wapinzani wanaojaribu kutaka kufika eneo hilo.

Ikumbukwe wakati Talibani walipoingia katika bonde hilo waliwahimiza wakazi wa eneo hilo kuendelea na shughuli zao za kawaida.

”Wanapaswa kutoka nje na kuendelea kufanya shughuli zao za kila siku,” alisema msemaji wa eneo hilo, Malavi Abdullah Rahamani.

Alisema kama ni wauzaji wanaweza kwenda kwenye maduka yao, ikiwa ni wakulima wanaweza kwenda kwenye mashamba yao, tuko hapa kuwalinda maisha yao na familia zao’.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!