Friday , 26 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Kimbunga chatikisa Texas, Louisiana
Kimataifa

Kimbunga chatikisa Texas, Louisiana

Spread the love

 

KIMBUNGA Nicholas kimetokea Texas nchini Marekani na kusababisha mvua kubwa, kuharibu miundobinu ya barabara na majengo. Anaripoti Glory Massamu, TUDARCo … (endelea).

Shule kadhaa katika majimbo ya Texas na Louisiana zimefungwa na mamia ya safari za ndege zimefutwa au kucheleweshwa katika viwanja vya ndege.

Kimbunga hicho kimetokea jana Jumatatu, tarehe 14 Septemba 2021 ambapo Rais wa Marekani, Joe Biden alitangaza hali ya dharura mjini Louisiana na kuamuru msaada kutolewa kwa maeneo yaliyoathirika.

Haya yanajiri wiki chache tu baada ya kimbunga Ida – ambacho ni cha tano kwa nguvu kuwahi kuikumba Marekani na kuwaacha zaidi ya wakaazi milioni moja wa Louisiana wakiwa hawana umeme.

Kituo cha Taifa cha Kimbunga cha Marekani kilionya athari za mafuriko ya kutishia maisha, hasa katika maeneo ya mji mkuu inaweza kutokea, hata hivyo Kituo cha Huduma ya Hali ya Hewa ya Taifa kilisema kuna hali ya kutishia maisha.

“Tunataka kuhakikisha kwamba hakuna mtu atayekutwa na dhoruba hii,” alisema Gavana wa Louisiana, John Edwards wakati akizungumza na waandishi wa habari

Kwa upande wake, Meya wa Houston, Sylvester Turner alionya juu ya mafuriko na kuwasisitiza wananchi wa jiji hilo kukaa mbali na barabara.

“Chukua vitu kwa umakini na ujiandae,” alisema Turner katika mkutano wa waandishi wa habari na kuongeza “hili ni tukio la mvua na hatujui ni mvua kiasi gani tutapata.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!