Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chadema wamng’ang’ania IGP Sirro, watoa ujumbe
Habari za SiasaTangulizi

Chadema wamng’ang’ania IGP Sirro, watoa ujumbe

Benson Kigaila, Naibu Katibu Mkuu Chadema Bara
Spread the love

 

CHAMA kikuu cha upinzani nchini Tanzania cha Chadema, kimewataka wadau mbalimbali wakiwemo vyama vya siasa, asasi za kiraia na vyombo vya habari kusimamia sheria za nchi ili zisivunjwe. Anaripoti Mwanaharusi Abdallah na Victoria Mwakisimba, TUDARCo … (endelea).

Pia, wamemtaka Inspekta Jenerali wa Polisi nchini humo (IGP) Sirro Sirro kujiuzulu au kuondolewa kwenye wadhifa huo na mamlaka yake ya uteuzi.

Hayo yamesemwa leo Jumanne, tarehe 14 Septemba 2021 na Benson Kigaila, Naibu Katibu Mkuu wa Chadema-Bara wakati anazungumza na waandishi wa habari, makao makuu ya chama hicho, Kinondoni mkoani Dar es Salaam, kuhusu kauli ya IGP Sirro aliyoitoa hivi karibuni.

Mara baada ya kurejea Tanzania kutoka katika ziara ya kikazi nchini Rwanda tarehe 10 Septemba 2021, IGP Sirro alisema katika ziara hiyo amejifunza namna jeshi la polisi la nchi hiyo linavyokabiliana na vitendo vya ugaidi na kuahidi kufanyia kazi mikakati yao hapa nchini ili kudhibiti vitendo hivyo.

“Tumeona wenzetu shule za dini, madrasa na sunday school kuna kikosi malaum kinapitia kuona mafunzo yanayotolewa je ni ya kizalendo au kuharibu nchi.”

“Tumeona ni uzoefu mzuri na sisi tushirikishe viongozi wa dini na timu ya kupambana na makosa ya ugaidi namna gani tupitie mafunzo ya kwenye dini shuleni hadi vyuo tuone mafunzo yanayotolewa ni kwa ajili ya kuwajenga au kuwabomoa vinana wa kitanzania,” alisema IGP Sirro.

Kutokana na kauli hiyo, Kigaila amesema, IGP Sirro anataka kuleta utaratibu ambao ni kinyume cha taratibu na kanuni za katiba ya nchi ambao ni kutembelea taasisi za kidini na kuangalia kama mafunzo yanayo tolewa ni ya uzalendo.

Amesema, anachokitangaza IGP Sirro kinakwenda kinyume cha katiba na sharia “kwa mujibu wa Katiba Ibara ya 19 katika kuenzi dini au kuendesha ibada majukumu hayo yatafanywa nje ya mamlaka.”

“Anachokifanya IGP Sirro ni ukikwaji wa katiba, tunatoa wito kwa taasisi za habari, vyama vya siasa, Watanzania, asasi za kiraina na taasisi za dini kuhakikisha wanailinda katiba na sheria ili isivunjwe.”

“Tusimame kwa pamoja kuitaka mamlaka ya uteuzi kumwondoa madarakani IGP Sirro kwani anachokifanya au anachotaka kufanya ni kuvunja katiba na sheria kitu ambacho kimekatazwa kwa kila mmoja wetu,” amesema Kigaila.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!