Tuesday , 7 May 2024
Home Kitengo Michezo Simba Bingwa, mara nne mfululizo
MichezoTangulizi

Simba Bingwa, mara nne mfululizo

Spread the love

 

MABAO mawili ya John Bocco na Chriss Mugalu yalitosha kuifanya Simba kutangazwa kuwa mabingwa wapya wa Ligi Kuu Tanzania Bara kwa msimu wa 2020/21 kwenye mchezo.dhidi ya Coastal Union. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea)

Mchezo huo ulipigwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam, kuanzia majira ya saa 1 usiku.

Baada ya kuchukua pointi tatu, sasa Simba itakuwa inafikisha alama 79, ambazo hazitafikiwa na timu yoyote kwenye msimamo wa Ligi.

Nafasi ya pili inashikiliwa na klabu ya Yanga, wenye pointi 70, hata wakishinda michezo yao miwili iliyosalia watafikisha pointi 76.

Huu utakuwa ubingwa wa nne mfululizo kwa klabu ya Simba toka msimu wa 2017/18, pia ubingwa huo utakuwa wa kwanza kwa kocha wa kikosi hiko Didier Gomes toka alipojiunga na klabu hiyo mwezi Januari.

Mabao ya leo ya Simba yalifungwa kwenye dakika ya 13 na Bocco, kupitia adhabu ndogo ya faulo na dakika 10 baade Mugalu alindika bao la pili na bao la 13 kwake kwa msimu huu, kwenye dakika ya 23

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

Michezo

Idris Sultan anogesha msimu wa 3 wa Bridgerton

Spread the loveSTAA wa burudani kutoka ardhi ya Tanzania, Idris Sultan amenogesha...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love JUMAPILI ya leo imekaa kipesa tuu yani baada ya...

error: Content is protected !!