Wednesday , 1 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais wa Haiti auawa katika shambulio
Kimataifa

Rais wa Haiti auawa katika shambulio

Spread the love

 

JOVENEL Moise (53), Rais wa Haiti ameuawa leo Jumatano, tarehe 7 Julai 2021, katika shambulio akiwa katika makazi yake. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).

Pia, katika shambulizi hilo, imeripotiwa Martine Moise, mke wa rais huyo, amejeruhiwa na amelazwa hospitalini.

Kaimu waziri mkuu wa nchi hiyo amesema, hatua zote zinachukuliwa “ili kuhakikisha serikali inaendelea.”

Moïse, amekuwa madarakani tangu Februari 2017, baada ya mtangulizi wake, Michel Martelly kung’atuka mamlakani.

Katika kipindi hicho cha utawala wake, Moise alikuwa akikabiliwa na tuhuma za ufisadi hali iliyosababisha maandamano ya mara kwa mara ya wananchi wa kupinga uongozi wake.

Katika maandamano ya mwaka 2019 ya kumpinga, Rais Moise, alisema “hatondoka nchini kwasababu ya shinikizo kutoka kwa magenge yaliyojihami na walanguzi wa dawa za kulevya.”

Mapema mwaka 2021, maandamano yalifanyika yakimtaka kujiuzulu nafasi hiyo kutokana na tuhuma mbalimbali.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!