Friday , 3 May 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Corona: Maambukizi mapya yashtua Uganda
Kimataifa

Corona: Maambukizi mapya yashtua Uganda

Spread the love

 

JUMLA ya watu 126 nchini Uganda wameripotiwa kufariki dunia ndani ya siku nne zilizopita kutokana na virusi vya corona (COVID-19). Inaripoti mitandao ya kimataifa…(endelea).

Idadi hiyo ni kubwa katika kipindi kichache ambapo mpaka sasa, watu waliofariki kutokana na ugonjwa huo wamefika 752.

Taarifa kutoka nchini humo zinaeleza, idadi kubwa ya watu wanaofikishwa hospitali kuopata huduma hiyo, wanakuwa katika hali mbaya jambo lililosababisha kuongezeka kwa vifo hivyo.

Dk Charles Olaro, Mkurugenzi wa Huduma za Matibabu Wizara ya Afya Uganda amesema “wimbi la tatu la corona ni baya zaidi na watu wana tabia ya kufika katika vituo vya afya wakiwa katika hali mbaya.”

Inaelezwa, vifo hivyo (126), ni asilimia 16.7 ya jumla ya vifo vilivyoripotiwa  nchini humo tangu ugonjwa huo kuingia Uganda mwaka jana.

Vifo hivyo ni sawa na asilimia 16.7 ya jumla ya vifo vilivyoripotiwa tangu kulipuka kwa ugonjwa huo mwaka 2020.

Taarifa kutoka Uganda zinaeleza, kati ya sampuli 7,196 zilizopimwa virusi vya corona tarehe 21 Juni 2021, watu 859 walikutwa na maambukizi. Idadi hiyo inafanya waliopimwa na kukutwa a corona kufika 74,260.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

error: Content is protected !!