Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Adhabu ya mkwepa kodi yaanikwa
Habari za Siasa

Adhabu ya mkwepa kodi yaanikwa

Dk. Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango
Spread the love

 

MFANYABIASHARA ama mtoa huduma ambaye atabainika kuwepa kulipa kodi, akikamatwa atalazimika kulipa asilimia 100 ya kodi aliyotakiwa kulipa kama adhabu. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Kwamba, kodi hiyo itakuwa mara mbili ya kodi anayodaiwa mteja, ambapo mapendekezo ya kuwekwa kwa adhabu hiyo yamefanywa na wabunge wa Bunge la Jamhuri.

Dk Mwigulu Nchemba, Waziri wa Fedha na Mipango akijibu hoja wakati wa kuhitimisha majadiliano ya Muswada wa Sheria ya Fedha ya mwaka 2021, amesema baada ya kusikia hoja za wabunge, serikali imeamua kuchukua ushauri kwa kuweka kifungu kipya cha kubana ukwepaji kodi.

Dk. Mwigulu amesema, makubaliano yaliyofikiwa katika kikao kati ya serikali na kamati ya bunge, ni kufanya mabadiliko kwenye tuliokuwa tumependekeza kuweka asilimia 75, wamependekeza kuwa asilimia 100 ya kodi iliyotakiwa kutozwa.

“Kwa maana hiyo, kodi itakuwa imezidishwa mara mbili ya iliyotakiwa kutozwa kama mtu huyo atakuwa amekwepa, kwa hiyo sisi kama serikali tunapokea maoni ya wa waheshimiwa wabunge na kamati ambayo ni mwakilishi wa Bunge,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!