Monday , 6 May 2024
Home Kitengo Maisha Afya COVID-19: Muhimbili yaweka sharti uvaaji barakoa
AfyaTangulizi

COVID-19: Muhimbili yaweka sharti uvaaji barakoa

Spread the love

 

HOSPITALI ya Taifa ya Muhimbili (MNH)- Upanga na Mlonganzila, Mkoa wa Dar es Salaam, imeweka sharti kwa wananchi, wafanyakazi na wanafunzi wanaokuwa maeneo ya hospitali hiyo, kuvaa barakoa wakati wote. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Lengo ni kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona (COVID-19).

Sharti hilo, limetolewa leo Jumanne, tarehe 22 Juni 2021 na Aminiel Aligaesha likiwa na lengo la kuhakikisha kila mmoja anachukua tahadhari ya kujikinga na kuwakinga wengine kuhusu corona.

“Kuvaa barakoa wakati wote wanapokuwa katika mazingira ya hospitali. Hakuna atakayeruhusiwa kuingia ndani ya eneo la hospitali bila kuvaa barakoa.


“Wafanyakazi wote na wanafunzi kuanzia sasa, wanapaswa kuvaa barakoa wakati wote wakiwa mazingira ya kazi. Hakuna mfanyakazi au mwanafunzi atakayeruhisiwa kutoa huduma kwa mgonjwa bila barakoa kuanzia kliniki, kwenye vipimo au wodini,” amesema Aminiel.

Aminiel amesema, watu wote wanaoingia maeneo ya hospitali, watapaswa kunawa mikono kwa kutumia sabuni na maji tiririka yaliyopo katika maeneo mbalimbali ya hospitali au vipukusi ‘sanitizer.’

“Eneo la Muhimbili lina msongamano, hivyo tunashauri idadi ya wasindikizaji kwa wagonjwa wanaokuja kliniki nayo kupungua hivyo mgonjwa ataruhusiwa kuja na msindikizaji mmoja,” amesema Aminiel na kuongeza:

“Wagonjwa waliolazwa wodini, wataruhusiwa kuonana na ndugu zao watano tu kwa siku ambapo asubuhi ni ndugu wawili, mchana mmoja na jioni wawili.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Jacob, Malisa wapandishwa kizimbani kwa mashtaka ya uongo mitandaoni

Spread the loveMKURUGENZI wa Shirika la Haki, Godlisten Malisa na mwanachama wa...

AfyaHabari Mchanganyiko

Huduma za kibingwa zazinduliwa katika hospitali za halmashauri 184

Spread the loveSERIKALI imezindua huduma za matibabu za kibingwa katika hospitali 184...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga Hidaya chatikisa Mafia

Spread the loveWAKATI hali ya upepo mkali ikiendelea kushuhudiwa katika baadhi ya...

error: Content is protected !!