Sunday , 28 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Mseven afunga shule, baa na makanisa Uganda
Kimataifa

Rais Mseven afunga shule, baa na makanisa Uganda

Spread the love

 

RAIS wa Uganda, Yoweri Museveni, ametangaza kufungwa kwa shule na taasisi za elimu ya juu na kusitisha mikusanyiko ya watu nchini humo kwa siku 42, kuanzia leo Jumatatu, tarehe 7 Juni 2021. Inaripoti Mitandao ya kimataifa … (endelea).

Ni baada ya nchi hiyo kukabiliwa na maambukizi mengi katika wimbi la pili la la ugonjwa wa corona (Covid-19).

Pia, baa na kumbi za sinema zimefungwa.

Tangazo hilo ni saa kadhaa baada ya wizara ya afya nchini humo, kutangaza maambukizi mapya 1,259 ya corona ambapo ni idadi kubwa zaidi ya maambukizo yaliyorekodiwa jana Jumapili, kwa siku moja na vifo tisa.

Amesema, usafiri wa umma nao utapigwa marufuku kuanzia Alhamisi ili kupisha wanafunzi ambao wako shuleni warudi nyumbani.

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni

Museveni amesema, walimu wote watapaswa kupewa chanjo kabla ya shule na vyuo kufunguliwa.

“Kuna ongezeko kubwa la maambukizi mashuleni tangu Mwezi Machi, wagonjwa 948 wameripotiwa kwenye shule 43 kutoka wilaya 22, naamini namba hii ni kubwa zaidi , shule zingine hazitoi takwimu kwa kuwa hawataki zifungwe na wengi wanawaza pesa tu” amesema Rais Museveni.

Hospitali ya rufaa ya Taifa ya Mulago, iliripoti kuongezeka kwa wagonjwa wa Covid-19 wiki iliyopita, ikisema inahitaji kuongeza vikitanda kwa ajili ya wagonjwa. hadi sasa, Uganda ina maambukizi 52,929 vya corona na vifo 374.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

error: Content is protected !!