Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais Mseven afunga shule, baa na makanisa Uganda
Kimataifa

Rais Mseven afunga shule, baa na makanisa Uganda

Spread the love

 

RAIS wa Uganda, Yoweri Museveni, ametangaza kufungwa kwa shule na taasisi za elimu ya juu na kusitisha mikusanyiko ya watu nchini humo kwa siku 42, kuanzia leo Jumatatu, tarehe 7 Juni 2021. Inaripoti Mitandao ya kimataifa … (endelea).

Ni baada ya nchi hiyo kukabiliwa na maambukizi mengi katika wimbi la pili la la ugonjwa wa corona (Covid-19).

Pia, baa na kumbi za sinema zimefungwa.

Tangazo hilo ni saa kadhaa baada ya wizara ya afya nchini humo, kutangaza maambukizi mapya 1,259 ya corona ambapo ni idadi kubwa zaidi ya maambukizo yaliyorekodiwa jana Jumapili, kwa siku moja na vifo tisa.

Amesema, usafiri wa umma nao utapigwa marufuku kuanzia Alhamisi ili kupisha wanafunzi ambao wako shuleni warudi nyumbani.

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni

Museveni amesema, walimu wote watapaswa kupewa chanjo kabla ya shule na vyuo kufunguliwa.

“Kuna ongezeko kubwa la maambukizi mashuleni tangu Mwezi Machi, wagonjwa 948 wameripotiwa kwenye shule 43 kutoka wilaya 22, naamini namba hii ni kubwa zaidi , shule zingine hazitoi takwimu kwa kuwa hawataki zifungwe na wengi wanawaza pesa tu” amesema Rais Museveni.

Hospitali ya rufaa ya Taifa ya Mulago, iliripoti kuongezeka kwa wagonjwa wa Covid-19 wiki iliyopita, ikisema inahitaji kuongeza vikitanda kwa ajili ya wagonjwa. hadi sasa, Uganda ina maambukizi 52,929 vya corona na vifo 374.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!